Advertisements

Wednesday, April 17, 2024

RAIS WA ZANZIBAR MHE.DK.HUSSEIN MWINYI AFUNGUA MKUTANO WA MAFUNZO KWA TAASISI ZA UKAGUZI NA MABUNGE YA SADCOPAC


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kuufungua Mkutano wa Mafunzo wa Kuwajengea Uwezo Taasisi za Ukaguzi na Mabunge ya (SADCOPAC) unaofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Uguja Jijini Zanzibar leo 17-4-2024

BAADHI ya Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Kamati mbalimbali za Bunge wakifuatila hutuba ya Ufunguzi wa Mkutano wa mafunzo ya kuwajengea uwezo pamoja na ufanyajikazi wa Taasisi za Ukaguzi na Mabunge ya (SADCOPAC) wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akifungua na kuufungua mkutano huo unaofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 17-4-2024
WASHIRIKI wa Mkutano wa Mafunzo wa kuwajengea uwezo pamoja na ufanyaji kazi wa Taasisi za Ukaguzi na Mabunge ya (SADCOPAC) wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia na kuufungua mkutano huo, unaofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 17-4-2024
BAADHI ya Makatibu Wakuu wa SMZ wakifuatilia hutuba ya ufunguzi wa Mkutano wa Mafunzo wa kuwajengea Uwezo Taasisi za Ukaguzi na Mabunge ya (SADCOPAC) wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia na kuufungua mkutano huo unaofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 17-4-2024

RAIS SAMIA AWASILI ANKARA UTURUKI KWA ZIARA RASMI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ankara Esenboga nchini Uturuki kwa ajili ya Ziara Rasmi tarehe 17 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ankara Esenboga nchini Uturuki kwa ajili ya Ziara Rasmi tarehe 17 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Waziri wa Familia na Huduma za Jamii wa Uturuki Mahinur Ozdemir Goktas mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ankara Esenboga nchini Uturuki kwa ajili ya Ziara Rasmi tarehe 17 Aprili, 2024.

SERIKALI YACHUKUA HATUA KULINDA BEI YA ZAO LA ALIZETI


Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali bungeni jijini Dodoma.

Na. Saidina Msangi, WF, Dodoma.
Serikali imesema kuwa imeweka kiwango maalumu cha ushuru wa forodha wa dola 500 za Marekani kwa kila tani moja ya ujazo kwenye mafuta ya kula kutoka nje ya nchi ili kulinda uzalishaji wa ndani.

Hayo yameelezwa bungeni, jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kiteto Mhe. Edward Olelekaita Kisau aliyetaka kujua kauli ya Serikali katika kulinda bei ya zao la alizeti kwa kuongeza kodi kwenye mafuta kutoka nje ya nchi.

Mhe. Chande alisema kuwa Serikali inatoza asilimia 0 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye mafuta ya kula yaliyozalishwa nchini kwa kutumia mbegu za mafuta ya kula, ikiwemo mbegu za alizeti ili kuhamasisha uzalishaji.

TANZANIA YAHIMIZA USHIRIKIANO NCHI ZA SADC KATIKA USIMAMIZI WA MISITU YA MIOMBO


Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo unaofanyika jijini Washngton DC nchini Marekani leo Aprili 17,2024.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo unaofanyika jijini Washngton DC nchini Marekani leo Aprili 17,2024.
Baadhi ya washiriki wakimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) (hayupo pichani) Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo unaofanyika jijini Washngton DC nchini Marekani leo Aprili 17,2024.
Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Deusdedith Bwoyo (kulia) akifuatilia matukio katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo unaofanyika jijini Washngton DC nchini Marekani leo Aprili 17,2024.

SERIKALI YABAINISHA MPANGO WA KUWASAIDIA WAJASIRIAMALI KUZALISHA BIDHAA BORA



NAIBU Waziri wa Viwanda na Biasha, Exaud Kigahe amebainisha mpango wa Serikali katika kuwasaidia wajasiriamali kuzalisha bidhaa bora ili kupata masoko ya uhakika.

Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalum, Ester Malleko ambaye alitaka kujua mpango wa Serikali wa kuwasaidia wajasiriamali kuzalisha bidhaa bora na kupata masoko ya uhakika.

Akijibu swalin hilo, Kigahe alisema Serikali imeweka mipango kadhaa ya kuwasaidia wajasiriamali kuzalisha bidhaa bora ili kupata masoko ya uhakika ikiwa ni pamoja na kupitia Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuwasaidia wajasiriamali wadogo kupata maeneo/majengo ya kuzalishia bidhaa zao, kuwapatia mitaji kupita Mfuko wa NEDF na nembo ya ubora wa bidhaa zao kwa miaka mitatu bila gharama.

Amesema pia kupitia SIDO, TBS na Wakala wa Vipimo (WMA) kuendelea kutoa mafunzo kwa wajasiriamali kuhusu kanuni za uzalishaji wenye tija, elimu ya utambuzi wa vifungashio na ufungashaji bora.

WAZIRI KAIRUKI KUMWAKILISHA RAIS SAMIA KWENYE MKUTANO WA KIMATAIFA WA MIOMBO WASHINGTON DC


Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) (kushoto) katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Dkt. Elsie Sia Kanza (kulia) alipowasili katika Ubalozi wa Tanzania Nchini Marekani uliopo jijini Washington DC
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) (kushoto) akijadili jambo na Balozi wa Tanzania Nchini Marekani, Mhe. Dkt. Elsie Sia Kanza (kulia) alipowasili katika Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani uliopo jijini Washington DC.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) (katikati) akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Ubalozi wa Tanzania Nchini Marekani uliopo jijini Washington DC Aprili 15,2024. Kulia ni Balozi wa Tanzania Nchini Marekani, Mhe. Dkt. Elsie Sia Kanza (kulia) na Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki, Wizara ya Maliasili na Utalii, Deusdedith Bwoyo (kushoto).

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki anatarajia kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo utakaofanyika Aprili 16-18 jijini Washington DC Marekani.

Mkutano huo pamoja na mambo mengine utajadili masuala mbalimbali ikiwemo namna ya kuimarisha mashirikiano na usimamizi wa misitu ya miombo kwa nchi wanachama za SADC, upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya usimamizi wa misitu ya miombo kwa nchi wanachama wa SADC, namna ya kuhama kutoka matumizi ya nishati chafu kwenda nishati safi pamoja na jinsi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika mifumo ya ikolojia na uhifadhi wa viumbe hai.

MATUMIZI YA TEKNOLOJIA YAHIMIZWA MKUTANO WA 10 WA WAKAGUZI AFRIKA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, akiwataka wakaguzi wa ndani barani Afrika kutumia utaalam wao wa ukaguzi kuzisaidia nchi zao kutatua chamgamoto, wakati wa Mkutano wa 10 wa Wakaguzi wa Ndani Barani Afrika, unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Na. Peter Haule, WF, Arusha.
Wakaguzi wa Ndani barani Afrika wametakiwa kubadilishana uzoefu na kutumia teknolojia katika kutatua changamoto mbalimbali katika taaluma yao na kuhakikisha wanasaidia taasisi na Serikali zao kuboresha ufanyaji kazi ili kuchochea maendeleo.

Hayo yameelezwa jijini Arusha na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Dkt. Saada Mkuya Salum, wakati wa Mkutano wa 10 wa Wakaguzi wa Ndani Barani Afrika, ulioanza kwa mikutano midogo inayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Dkt. Mkuya alisema kuwa mkutano huo umewakutanisha wakaguzi kutoka nchi 27 za Afrika na kwamba mkutano huo ni jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu ambapo wageni watajifunza Tanzania na wageni watajifunza kwa wenzao kwa kuwa mazingira ya ukaguzi yamebadilika kutokana na kuimarika kwa teknolojia duniani.

KIKWETE AWAASA VIJANA KUWA CHACHU YA UTENGAMANO WA KIKANDA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI


Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia jambo kabla ya kuhutubia katika mkutano mkuu wa kwanza wa marais na viongozi wa sasa na wa zamani wa serikali za wanafunzi wa vyuo vikuu vya Uganda ambapo alialikwa kama mgeni rasmi jana Jumatatu.
Makamu wa Rais wa Uganda, Bi. Jessica Allupo akifuatilia hotuba ya Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika mkutano mkuu wa kwanza wa marais na viongozi wa sasa na wa zamani wa serikali za wanafunzi wa vyuo vikuu vya Uganda.
Wahudhuriaji katika katika mkutano mkuu wa kwanza wa marais na viongozi wa sasa na wa zamani wa serikali za wanafunzi wa vyuo vikuu vya Uganda ambapo alialikwa kama mgeni rasmi.

CDE. MBETO ATAKA VIWANJA VIWANJA VYA MICHEZO ZANZIBAR VITUMIKE


Na Mwandishi Wetu -Zanzibar.
KATIBU wa Kamati Maalum ya NEC,Idara ya Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Zanzibar Khamis Mbeto Khamis,ameishauri Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Zanzibar kuhakikisha inasimamia vizuri matumizi ya Viwanja vya vya kisasa vya michezo vilivyojengwa na Serikali kwa ajili ya kukuza vipaji vya Vijana kupitia michezo mbalimbali nchini.

Ushauri huo aliutoa wakati akizindua msimu wa nne wa ligi ya mpira wa miguu ya Mwakilishi wa Jimbo la Mwanakwerekwe Mhe.Ameir Abdalla Ameir "Ameir CUP" iliyozinduliwa katika Uwanja wa Magirisi Unguja.

Amesema Serikali imejenga viwanja vya kisasa kwa kutoa kipaumbele cha kukuza sekta ya michezo nchini.

Katika maelezo yake Mbeto,alisema suala la michezo limepewa nafasi kubwa ndani ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 ili Wananchi hasa vijana waweze kujiajiri wenyewe kupitia sekta hiyo.

Katibu huyo wa Kamati Maalum Mbeto,alieleza kuwa Wizara ya Habari kupitia Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) wanatakiwa kuhakikisha ligi mbalimbali zinazochezwa katika viwanja vya mitaani na zina mashabiki wengi zinachezwa katika viwanja vya kisasa ili kiibua vipaji na kuongeza kipato.

WAZIRI MKUU : MAHAKAMA ZAANZA KUTUMIA MFUMO WA KUTAFSIRI LUGHA ZA KIINGEREZA NA KISWAHILI

*Nia ni kuwawezesha wananchi kuelewa mwenendo wa mashauri

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihitimisha hoja ya bajeti Ofisi ya Waziri Mkuu, taasisi zake, na mfuko wa Bunge kwa mwaka 2024/2025, bungeni jijini Dodoma

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Mahakama zimeanza kutumia mfumo unaonasa sauti na kuzibadilisha kwenda kwenye maandishi huku ukitafsiri lugha za Kiingereza na Kiswahili.

“Hii ni hatua kubwa sana kwani mfumo huo unarekodi sauti na kupeleka kwenye maandishi. Vilevile, unaweza kutafsiri lugha ya Kiswahili au Kiingereza kulingana na uhitaji,” amesema na kuongeza: “Kanuni za Mahakama zimeanza kutafsiriwa sambamba na uandaaji wa mihutasari ya hukumu kwa Kiswahili ili kuwawezesha wananchi kuelewa mwenendo wa mashauri.”

Ametoa kauli hiyo jioni (Jumatatu, Aprili 15, 2024) Bungeni, jijini Dodoma wakati akitoa hoja ya kuhitimisha mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2024/2025.

Akielezea mambo yaliyofanyika ndani ya miaka mitatu ya Serikali ya awamu ya sita, Waziri Mkuu amesema mbali ya matumizi ya Kiswahili mahakamani, Serikali imeendelea kuimarisha matumizi ya TEHAMA ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia kutokana na mapinduzi ya nne ya viwanda duniani.

RAIS SAMIA ATOA TANI 189 ZA MBEGU – WAZIRI MKUU


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia ameridhia kutoa tani 189 za mbegu za mpunga, mahindi na alizeti ili zisambazwe kwa wakulima wa wilaya ya Kilombero.

“Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatoa pole kwa wananchi wote walioathirika na mafuriko yaliyotokana na mvua zinazonyesha nchini, lakini pia ametoa mbegu hizo ili kuhakikisha wale waliopata athari katika mashamba yao waweze kuendelea na shughuli za kilimo pale hali itakapokaa sawa,” amesema.
Ameyasema hayo (Jumanne, Aprili 16, 2024) wakati akizungumza na wananchi wa maeneo ya Mlimba, Taweta, Masagati wilayani Kilombero, mkoani Morogoro ambako alikwenda kukagua athari za mafuriko.

Waziri Mkuu ambaye pia alikagua bonde la mto Kilombero linalojumuisha wilaya tatu za Kilombero, Ulanga na Malinyi, amesema Rais Samia ameelekeza Serikali iendelee kuwahudumia wananchi wote waliopata athari ikiwemo kuimarisha maeneo ya utoaji huduma za afya, kugawa vyakula na kurejesha miundombinu ikiwemo barabara na reli.

Tuesday, April 16, 2024

TCAA YAPONGEZWA USIMAMIZI THABITI SEKTA YA USAFIRI WA ANGA



Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Bw. Daniel Malanga akiwasilisha majukumu ya Mamlaka mbele ya Kamati ya Mawasiliano Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilshi Zanzibar lipotembelea Makao Makuu ya TCAA kujionea na kujifunza shughuli za usimamizi wa sekta ya usafiri wa anga nchini.
Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilshi Zanzibar Yahya Rashid Abdallah akizungumza mara baada ya kamati hiyo kupata taarifa ya kazi zinazofanywa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).
Baadhi ya wanakamati ya Mawasiliano Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilshi Zanzibar  wakiuliza maswali mara baada ya kupata maelezo kuhusu kazi zinazofanywa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) walipotembelea makao makuu wa Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam.

DKT. TULIA AKIFUNGUA KIKAO CHA MABADILIKO YA TABIANCHI




Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, akifungua kikao cha kujadili changamoto za mabadiliko ya tabianchi yanayoikumba Dunia na utatuzi wake, wakati wa Mkutano wa Mwaka 2024 wa Jukwaa la Kibunge la Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani unaofanyika katika Makao Makuu ya Benki ya Dunia, Washington DC, nchini Marekani leo tarehe 16 Aprili, 2024.



PICHA NA OFISI YA BUNGE

DKT. KIKWETE ATEMBELEA CHUO CHA UONGOZI CHA JULIUS NYERERE KILICHOPO NDANI YA CHUO KIKUU CHJA MAKERERE JIJINI KAMPALA, UGANDA



Rais Mstaafu Dkt. Kikwete akiwa na Mkurugenzi wa Kituo cha Uongozi cha Julius Nyerere, Dkt. Nansozi Muwanga alipotembelea Kituo hicho kilichopo ndani ya Chuo Kikuu cha Makerere, Kampala, Uganda, jana Jumatatu.

Kituo hicho, kinachotoa mafunzo ya uongozi na kuandaa vijana kuwa viongozi bora, kinaratibiwa na chuo Kikuu cha hicho kikongwe Afrika Mashariki.

Dkt Kikwete alitembelea chuoni hapo alipoalikwa kama mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa kwanza wa marais na viongozi wa sasa na wa zamani wa serikali za wanafunzi wa vyuo vikuu vya Uganda ambapo alialikwa kama mgeni rasmi. Mkutano huo, uliojadili umuhimu na nafasi ya viongozi waliopo madarakani kuandaa viongozi wanaochipukia, ulihudhuriwa na zaidi ya marais na viongozi wa sasa na waliowahi kuwa viongozi wa serikali za wanafunzi wa vyuo vikuu vya nchini Uganda zaidi ya 1,000.

RAIS SAMIA ASHIRIKI MSIBA WA MZEE MUSSA ABDULRAHMAN, UNGUJA ZANZIBAR


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpa pole na kumfariji Bi. Mwanakheri Mussa Yussuf, Mjane wa Marehemu Mzee Mussa Abdulrahman ambaye alikuwa rafiki wa familia na Jirani wa karibu aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo mtaa wa Mombasa, Zanzibar. Rais Samia alifika kutoa pole msibani Kwahani Mchangamwingi Zanzibar tarehe 16 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimfariji Bi. Mwanakheri Mussa Yussuf, Mjane wa Marehemu Mzee Mussa Abdulrahman ambaye alikuwa rafiki wa familia na Jirani wa karibu aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo mtaa wa Mombasa, Zanzibar, kushoto ni Mtoto wa Marehemu Bi. Fatma Mussa Abdulrahman. Rais Samia alifika kutoa pole msibani Kwahani Mchangamwingi Zanzibar tarehe 16 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiomba dua pamoja na Wanafamilia wa Marehemu Mzee Mussa Abdulrahman aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo mtaa wa Mombasa, Zanzibar. Rais Samia alifika kutoa pole msibani Kwahani Mchangamwingi Zanzibar tarehe 16 Aprili, 2024.

MILIONI 100 KUTUMIKA KUONGEZA MAJENGO ZAHANATI YA MADOPE,LUDEWA

NAIBU Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe Dkt Festo Dugange amesema katika mwaka wa fedha 2025/26 Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa itatenga Sh Milioni 100 kwa ajili ya kuongeza majengo na kuanza utaratibu wa kupandisha hadhi zahanati ya Madope kuwa kituo cha afya.

Mhe Dkt Dugange ametoa kauli hiyo leo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Ludewa, Mhe Joseph Kamonga aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kupandisha hadhi Zahanati za Madope na Ludewa kuwa vituo vya afya.

“ Zahanati za Madope na Ludende ni Zahanati zilizopo kwenye Makao Makuu ya Kata za Madope na Ludende Mtawalia. Zahanati ya Madope ina eneo la takribani ekari 10 pamoja na vigezo vingine inakidhi kuwa na kituo cha afya.

Katika mwaka wa fedha 2025/26 serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo itatenga Sh Milioni 100 kwa ajili ya kuongeza majengo na kuanza utaratibu wa kuipandisha hadhi kuwa kitio cha afya,” Amesema Mhe Dkt Dugange.

TAMISEMI, WIZARA YA ELIMU KUWAKWAMUA WANAFUNZI WALIOKWAMA NA MAFURIKO

KUTOKANA na hali ya mafuriko yanayoendelea, Ofisi ya Rais-TAMISEMI na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia zimekubaliana namna ya kuwasaidia wanafunzi waliokwa kuendelea na masomo ili waendelee na masomo.
Akizungumza leo mara baada ya kikoa kilichowakutanisha mawaziri na walaamu wa wizara hizo mbili, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mohamed Nchengerwa amesema kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha kuna baadhi ya wanafunzi wameshindwa kuendelea na masomo kutokana na changamoto ya mafuriko.
“Kutokana na hali ya mfuriko yanayoendelea nchini, mimi na mwenzangu wa wizara ya elimu (Profesa Adolf Mkenda) tumekubaliana sasa tunakazi ya kuja na mpango wa muda mfupi na muda mrefu ambao utawawezesha vijana wetu wanaosoma shule mbalimbali ambao leo hii wamekwama kuendela na masomo kwasababu ya majanga ya mafuriki yanayoendelea kote nchini hususani katika mikoa ya Pwani, Morogoro, Katavi na mikoa ya kaskazini na kusini.”

Amesema katika kutekeleza hilo wizara zimewaelekeza wataalamu kutoka wizara hizo kwenda nchi nzima kufanya tathimini na kujiridhisha kutokana na uharibifu mkubwa wa miundombinu ya shule uliochangiwa na mafuruki.

KINANA AKEMEA UKABILA,ASHAURI VIONGOZI WACHAGULIWE KWA SIFA

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Tanzania Bara Abdulrahman Kinana amekemea tabia ya baadhi ya wanaCCM na wananchi kuendekeza ukabila na kwamba ukabila ni jambo ambalo limepitwa na wakati na halina tija katika Taifa.

Amesisitiza hakuna faida yeyote ambayo inapatikana kwa kuendekeza ukabila zaidi ya kuleta mgawanyiko katika Taifa huku akifafanua Hayati Baba wa Taifa Mwalim Julius Nyerere alikemea ukabila.

“Kuwa na makabila ni jambo la kawaida ila ukabila ni jambo baya na kwamba kumuhukumu mtu kwa jambo ambalo hana uwezo nalo sio sahihi.”
Kinana aliyekuwa akizungumza na wanachama wa CCM Wilaya ya Rorya mkoani Mara moja ya malalamiko aliyopewa ni kuwepo kwa ukabila ka baadhi ya wanaCCM katika wilaya hiyo.

Hivyo wakati anazungumzia malalamiko hayo Makamu Mwenyekiti Kinana ameeleza Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alitoka katika kabila dogo mkoani hapa lakini aliongoza nchi kwa miaka 24, alipendwa, aliheshimiwa, alithaminiwa si kwa sababu ya ukabila bali kutokana na kazi nzuri aliyoitenda kwa uadilifu na kuheshimika Tanzania, Afrika na duniani kote.

WAHITIMU WA MASOMO YA SHERIA NCHINI WASISITIZWA KUWA NA UTAMADUNI WA KUJISOMEA


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma, akizungumza wakati akiongoza maadhimisho ya Siku ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) yaliyofanyika Leo Aprili 15,2024 jijini Dodoma.
Makamu Mkuu wa Chuo cha UDOM Prof. Lughano Kusiluka akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) yaliyofanyika Leo Aprili 15,2024 jijini Dodoma.
Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma (hayupo pichani), wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) yaliyofanyika Leo Aprili 15,2024 jijini Dodoma.

Na Gideon Gregory, Dodoma.
Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma amewasisitiza wanafunzi wanaohitimu masomo ya Sheria nchini kuwa na utamaduni wa kujisomea kwani kwasasa dunia inapitia mabadiliko makubwa ya matumizi ya Teknolojia kwenye utendaji wa kazi.

Jaji Mkuu ameyasema hayo Aprili 15,2024 Jijini Dodoma wakati akiongoza maadhimisho ya Siku ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambapo yameongozwa na kauli mbiu isemayo “Uimarishwaji wa kliniki za sheria vyuo vikuu katika kukuza na kupanua wigo wa upatikanaji wa haki Tanzania”.

Monday, April 15, 2024

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA KONGAMANO LA KUHAMASISHA UWEKEZAJI BUSTANI ZA KIJANI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa na viongozi mbalimbali katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gaspar mkoani Dodoma alipowasili kwaajili ya kufungua Kongamano la Kuhamasisha Uwekezaji katika Bustani za Kijani Nchini kwa Maendeleo Endelevu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akifuatilia mawasilisho mbalimbali wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la Kuhamasisha Uwekezaji katika Bustani za Kijani Nchini kwa Maendeleo Endelevu linalofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gaspar mkoani Dodoma tarehe 15 Aprili 2024. Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Selemani Jafo na kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI Bw. Kadari Singo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la Kuhamasisha Uwekezaji katika Bustani za Kijani Nchini kwa Maendeleo Endelevu linalofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gaspar mkoani Dodoma