Advertisements

Thursday, December 7, 2017

Fundisho la wiki' Dada Jasmini! alivyo vuka majaribu ya kusalitiwa na Mume!

Inatia huruma kwa Dada Jasmini Shabani aliye kutikana maeneo ya Buguruni Rozana, ambaye kapitia majaribu na misukosuko katika maisha ya ndoa yake, ikiwa ni pamoja na kusalitiwa na Mume wake wa kwanza pindi alipokuwa na ujauzito wa miezi mitano.

Katika maisha ya ndoa kuna changamoto nyingi zinazo sikitisha lakini kwa upande mwingine zinazo chekesha. Amini  ukisema Ndoa ni sawa na neno SIRI maana yaliyomo ndani Mungu ndio anajua unaweza ukakutana na wanandoa yaani Mke na Mume wameongozana wakiwa na nyuso za furaha kumbe mioyo yao haipatani kama Chui na Mbuzi.


Ukifikiria sana ndoa unaweza sema labda ndoa nyingi huwa zinatokea kama ajali, yaani utafikiri wanalazimishwaga. Kiukweli usipo lizika na uliye mchagua sasa huwezi kulizika maisha yako yote. Mpende mwenzio kama ujipendavyo hata vitabu vya mungu viliandika.

No comments: