Advertisements

Saturday, January 13, 2018

WAZIRI UMMY ASHUHUDIA COASTAL UNION IKIILAZA KURUGENZI YA MUFINDI MABAO 3-0 DAKIKA 45 ZA KIPINDI CHA KWANZA LEO

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mchezo baina ya Coastal Union na Kurugenzi ya Mufundi akifuatilia mchezo huo katikati akiwa na Jezi ya Coastal Union kushoto ni Mwenyekiti wa timu ya Coastal Union Steven Mguto na Kulia ni Katibu wa Chama cha Soka Mkoa wa Tanga(TRFA) Beatrice Mgaya (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha 
Sehemu ya mashabiki wa soka mkoa wa Tanga wakiojitokeza kufuatilia mchezo huo 
Wachezaji wa timu ya Coastal Union wakishangilia moja ya bao nne ambazo walifunga wakati wa kipindi cha dakika 45 za kwanza kabla ya kuanza kipindi cha pili ambapo Coastal Union ilikuwa ikiongoza kwa mabao 3-0
Mchezaji wa timu ya Coastal Union Raizani Hafidhi kushoto akijaribu kumtoka wa timu ya Kurugenzi FC ya Mufindi Nickraus Mwansumbule wakati wa mchezo wa Ligi Daraja la kwanza uliochezwa leo kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga ambapo mpaka dakika 45 Coastal Union walikuwa wakiongoza kwa mabao 3-0

No comments: